Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Marasimu ya kihistoria ya mazishi ya mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Hussein Khamenei (Allah Amrehemu), pamoja na miili ya mashahidi wa familia yake, yanafanyika leo nchini Iraq.

Waombolezaji kutoka maeneo mbalimbali ya Iraq na mataifa mengine wamejitokeza kwa wingi kushiriki katika shughuli hizo za kutoa heshima za mwisho kwa Kiongozi huyo, ambaye alitambulika kwa mchango wake katika kuimarisha umoja wa Umma wa Kiislamu, kutetea wanyonge na kusimamia misingi ya Mapinduzi ya Kiislamu.

Marasimu hayo yanajumuisha kupitishwa kwa msafara wa mazishi katika maeneo matakatifu ya Iraq, huku maelfu ya waumini wakishiriki katika dua, maombolezo na ibada mbalimbali za kumuombea marehemu.


Sheikh Ibrahim Zakzaky, Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Nchini Nigeria, ameshiriki pamoja na Waombolezaji wengine Nchini Iraq katika Kutoa Heshima zao za Mwisho kwa Kiongozi wa Umma Ayatollah Sayyid Ali Hussein Khamenei (ra).




Umati wa Waombolezaji Katika Mji wa Najaf, waliojitokeza kwa wingi katika Marasimu ya Mazishi ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (ra).

Your Comment